Home Soka Sadney Amaliza Mchezo Kirumba

Sadney Amaliza Mchezo Kirumba

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji Mnamibia wa klabu ya Yanga hatimaye amefunga goli lililoipa klabu yake ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbao Fc katika uwanja wa Ccm Kirumba jijini Mwanza.

Mbao licha ya kuwa nyumbani wamekubali kipigo hicho baada ya kuruhusu goli dakika ya 62 baada ya mabeki wa timu hiyo kushindwa kuokoa krosi ya Balama Mapinduzi aliyekua mwiba katika mchezo wa leo.

Yanga walijitahidi kupeleka mashambulizi langoni kwa mbao ambapo umakini mdogo wa Molinga na Sadney uliwakosesha mabao kadhaa licha ya Molinga kupata nafasi za kupiga mipira ya faulo.

banner

Kwa ushindi huo Yanga imefikisha alama saba baada ya kucheza michezo minne na itashuka tena dimbani hapo kuwakabili Pyramids Fc katika mchezo wa ligi ya kuwania kufuzu makundi kombe la shirikisho barani Afrika.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited