Home Soka Fernandes Aing’arisha Man Utd

Fernandes Aing’arisha Man Utd

by Sports Leo
0 comments

Kiungo mpya wa klabu ya Manchester United Bruno Fernandes ameendelea kung’ara katika kikosi cha timu hiyo baada ya jana kuisaidia kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Watford katika mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza.

Bruno alifanikiwa kufunga bao lake la kwanza la Epl kwa penati dakika ya 42 baada ya Golikipa wa Watford kumuangusha ndani ya mita 18.

Pia kiungo huyo alifanikiwa kuweka assisti yake ya pili na tatu baada ya kumpa pasi Antonio Martial aliyefunga bao la pili na Mason Greenwood aliyefunga la tatu.

banner

Man united imefikisha pointi 41 nyuma ya Chelsea iliyo nafasi ya nne huku Liverpool wakiwa kileleni mwa msimamo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited