Home Makala Mabondia 20 Kuchujwa Mwanza

Mabondia 20 Kuchujwa Mwanza

by Sports Leo
0 comments

Siku ya kesho Jumamosi mabondia 20 watazichapa katika pambano la kuwapata mabondia nane watakaoiwakilisha Mwanza kwenye mashindano ya ngumi za ridhaa Taifa tarehe 25 March mkoani Tanga.

Jopo la makocha wamejiandaa vyema kuchagua mabondia wazuri watakaowachuja na kuwaingiza kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano hayo ya kuuwakilisha mkoa wa Mwanza.

Katibu wa chama cha ngumi za ridhaa wilaya ya Nyamagana ,Hamad Mabula amesema kuwa pambano hilo litafanyika  ukumbi wa Bundasliga uliopo eneo la Nyasaka na mabondia wote wameshakamilisha kupima uzito pamoja na afya zao tayari kabisa kwa pambano hilo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited