Mechi ya watani wa jadi Yanga vs Simba iliyochezwa Jumapili Machi 8, 2020 imevunja rekodi ya mapato kwa kuiingizia serikali shilingi milioni 153.2 kiasi ambacho hakijawahi kupatikana katika historia ya mechi za watani hao.
Taarifa hiyo imetolewa mapema leo na Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbas wakati akiongea na vyombo vya habari mjini Dodoma.
Aidha ukiondoa mapato ya Serikali, jumla ya Tsh Milioni 545.4 zilikuwa ni mapato ya timu (Yanga) ambao walikuwa wenyeji wa mchezo huo uliofanyika machi 8 mwaka huu.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Hii ni rekodi mpya katika historia ya uwanja huo uliozinduliwa mwaka 2007 ukilinganisha na mechi zingine zilizochezwa uwanja hapo zikiwemo za kimataifa.