Home Soka “Tukipata Wanne Fresh”-Scholes

“Tukipata Wanne Fresh”-Scholes

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa zamani wa Man Utd Paul Scholes anaamini kwamba Manchester United bado inahitaji wachezaji wengine wasiopungua wanne ili kuwa kwenye viwango vya kuchuana Liverpool kwenye Ligi Kuu England, licha ya staa wao mpya, Bruno Fernandes kufanya maajabu tangu alipotua Old Trafford Januari.

“Bado nadhani kuna wachezaji wanahitaji. Wameonekana wazuri kwa siku za karibuni tangu alipokuja Fernandes, lakini Liverpool na Man City wapo mbali sana,” Alisema kiungo huyo ambae wakati anacheza hakua na wakala wa kumsimamia.

Mastaa kibao wamehusishwa kuhitajika Old Traffod kwenda kujenga kikosi cha kurudisha zama za ushindi klabuni hapo kama Jadon Sancho,Thomas Weimer,Harry Kane na wengineo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited