Home Soka Mbao Mwendo Mdundo

Mbao Mwendo Mdundo

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Mbao Fc ya jijini Mwanza imeendelea kupata ushindi baada ya kuifunga Namungo Fc mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa jijini Mwanza.

Mabao ya Mbao Fc yalifungwa mapema kipindi cha kwanza kupitia kwa Jordan John dakika ya 4 na 14 huku Abdulkareem Segeja akifunga bao la tatu dakika ya 28 na kuipa Mbao Fc ushindi wa saba mfululizo na kuelekea kuepuka kushuka daraja.

Mbao imeendeleza matokeo ya ushindi chini ya kocha Fred Felix Minziro ambaye aliletwa ili kuinusuru timu hiyo isishuke daraja ambapo sasa imefikisha alama 42 nafasi ya 16 ya msimamo wa ligi kuu Tanzania bara.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited