Home Makala Ndayiragije Atemwa Stars

Ndayiragije Atemwa Stars

by Sports Leo
0 comments

Taarifa za awali zinadai kuwa shirikisho la soka nchini Tanzania lipo mbioni kumtema kocha wa timu hiyo Ettiene Ndayiragije baada ya kuwa na mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha hasa katika michuano ya Chan 2021 nchini Cameroon.

Ingawa bado shirikisho hilo halijathibitisha taarifa hizo lakini tayari lipo mbioni kumuajiri aliyekuwa kocha wa zamani wa timu hiyo Kim Poulsen huku likificha kuwa anaajiri kwa nafasi ipi katika kocha wa vijana ama timu kubwa.

Wadau wengi wa soka hapa nchini wamekua wakikosoa mbinu za Ettiene aliyewahi kuzifundisha timu za Mbao Fc na Azam Fc hasa katika uchaguzi wa kikosi ambapo hivi karibuni aliwatema baadhi ya mastaa na kuita wachezaji wachanga katika kikosi cha Chan.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited