Home Soka Molinga Ajiunga Namungo Fc

Molinga Ajiunga Namungo Fc

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Yanga sc David Molinga ‘Falcao’amejiunga na Namungo Fc inayoshiriki ligi kuu nchini baada ya kumalizana na timu ya Zesco United nayoshiriki ligi kuu ya nchini Zambia.

Awali kabla ya kujiunga na Zesco United Molinga alicheza Yanga sc na kuwa kipenzi cha mashabiki akifunga mabao 12 kwa msimu wa ligi kuu 2019/2020 lakini Yanga sc waliamua kumuacha na kusajili majembe mapya wakina Michael Sarpong na Yacouba Sogne.

Inadaiwa Namungo Fc imekamilisha usajili wa Molinga ambae atakuja kuungana na Obrey Chilwa na Steven Sey pamoja na Bigirimana Blaize katika safu ya ushambuliaji klabuni hapo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited