Home Soka OLE BADO YUPO SANA OLD TRAFFORD

OLE BADO YUPO SANA OLD TRAFFORD

by Sports Leo
0 comments

Uongozi na vigogo wa Man Utd ukiongozwa na Sir Alex Ferguson umempa nafasi ya mwisho mkufunzi wa timu hiyo Ole kuiongoza katika michezo kadhaa ijayo.
(chanzo:skysports)

Solskjaer anazidi kuwa kwenye presha ya kuendelea kuwepo Old Trafford na amepewa mchezo wa Jumamosi dhidi ya Tottenham Hotspurs kujaribu kubadili hali ya hewa na kutetea kibarua chake.

Man Utd imekusanya alama moja tu kati ya michezo mitano iliyopita ya ligi kuu nchini Uingereza ikipokea kipigo kizito cha 5-0 nyumbani Old TRafford dhidi ya Liverpool.

banner

Antonio Conte anatajwa ataenda kuwa mrithi endapo Solskjaer akifukuzwa.Conte amekuwa hapendi kuchukua timu katikati ya msimu lakini ukubwa na ndoto ya kuifundisha Man Utd ndiyo kitu pekee kinachoweza kumbadilisha mawazo yake.

Conte anaamini kwa kikosi cha sasa cha Man Utd anaweza kuipa timu hiyo mafanikio ndani ya msimu huu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited