Home Soka MBWANA SAMATTA AMTAJA MWENYE TUZO YA UFUNGAJI BORA UBELGIJI

MBWANA SAMATTA AMTAJA MWENYE TUZO YA UFUNGAJI BORA UBELGIJI

by Sports Leo
0 comments

NAHODHA wa timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta anayekipiga KRC Genk ameweka bayana kwamba yeye sio mfungaji bora kwenye ligi ya Ubelgiji badala yake alikuwa akimpa changamoto mfungaji bora wa msimu uliopita.
Samatta ambaye ametia timu bongo na alipokelewa kwa heshima na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo,Dk. Harrison Mwakyembe, usiku wa kuamkia Jumapili.
"Sina tuzo ya mfungaji bora kwenye Ligi Kuu ya Ubelgiji msimu huu, mfungaji bora ni Hamdi Alboui huyu tulikuwa tunashindana naye ila yeye ametupia mabao 25 mimi nina mabao 23.
"Nafikira mimi ndiye nilikuwa nampa changamoto kwani yeye ndiye alikuwa mfungaji bora msimu uliopita, kwa hiyo nilikuwa najaribu kumvua ubingwa haikuwa bahati," amesema Samatta.
Samatta mkononi mwake ana tuzo ya kiatu cha Mchezaji Bora wa Mwaka Mwenye Asili ya Afrika 'Ebony Shoe'.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited