Home Makala Aucho,Saidoo Majanga Yanga sc

Aucho,Saidoo Majanga Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc itawakosa mastaa wake Khalid Aucho,Saido Ntibanzokiza na Djuma Shabani kutokana na sababu za kiafya ikiwemo majeraha na kuumwa ugonjwa wa maralia kuelekea katika mchezo wa kesho wa ligi kuu dhidi ya Geita Gold Fc.

Mchezo huo utakaofanyika katika uwanja wa Ccm Kirumba jijini Mwanza umekua gumzo kutokana na baadhi ya sekeseke ikiwemo kulalamika kwa mashabiki wa Geita Gold Fc kuwa wamehujimiwa kutokana na uongozi wa klabu hiyo kuuhamishia mchezo Mwanza mjini kutoka katika uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita.

Yanga sc itawakosa mastaa hao muhimu kikosini kutokana na mchango wao siku za karibuni huku Saido na Aucho wakiwa na majeraha na Djuma akisumbuliwa na maralia.

banner

Yanga sc inawabidi washinde mchezo huo ili kujitengenezea mazingira ya ubingwa mapema kwani mpaka sasa wanaongoza kwa tofauti ya alama nane pekee dhidi ya Simba sc anayeshika nafasi ya pili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited