Home Makala Al Ahly Wafanya Kufuru kwa Tau

Al Ahly Wafanya Kufuru kwa Tau

by Sports Leo
0 comments

Mazungumza ya kuongeza mkataba mpya baina ya klabu ya Al Ahly na mshambuliaji Percy Tau yamefikia pazuri ambapo staa huyo anatarajiwa kusaini mkataba mpya wa kuendelea kukipiga klabuni hapo kwa miaka mitatu mingine huku akitarajiwa kuwa mchezaji anayelipwa zaidi barani Afrika.

Katika mkataba huo mpya Tau atakua anatia mfukoni Mshahara wa dola milioni 5.13 katika misimu mitatu (3) ijayo ambazo ni zaidi ya Shilingi Bilioni 13 za Kitanzania.

Mishahara ya kila mwaka akiwa na klabu hiyo ilikuwa ni dola milioni 1.2 ikiwa ni zaidi ya Shilingi Bilioni 3 kwa Mwaka na sasa itaongezeka hadi dola milioni 1.3 (zaidi ya shilingi Bilioni 3.3 za Kitanzania) katika mwaka wa kwanza, dola milioni 1.4 (zaidi ya Shilingi Bilioni 3.7) kwa mwaka wa pili na dola milioni 1.6 (zaidi ya Shilingi Bilioni 4) kwa mwaka wa tatu.

banner

Kwenye Mkataba huo wa Tau inamaanisha mwaka wa mwisho atakuwa anapokea mshahara wa shilingi Milioni 340 kwa mwezi ambapo kwa wiki atakuwa analamba Milioni 85,Milioni 12 kwa siku.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited