Home Makala Al Hilal Fc Yamuaga Rasmi Ibenge

Al Hilal Fc Yamuaga Rasmi Ibenge

Klabu ya Al Hilal Omdurman ya nchini Sudan imethibitisha kuachana na kocha wake Florent Ibenge

by Dennis Msotwa
0 comments
Al Hilal - sportsleo.co.tz

Klabu ya Al Hilal Omdurman ya nchini Sudan imethibitisha kuachana na kocha wake Florent Ibenge baada ya miaka mitatu ya kufanya kazi na klabu hiyo kubwa nchini humo.

Timu hiyo imeachana na Ibenge baada ya makubaliano ya pande mbili kufuatia mkataba wa kocha huyo kufika mwishoni na kuamua kitoongeza tena.

Taarifa za ndani kutoka nchini Tanzania zinadai kuwa kocha huyo atatangazwa kuwa kocha wa Azam FC siku chache zijazo baada ya kukubali ofa ya vigogo hao wa Chamazi.

banner

Kocha huyo alikua hapa nchini siku chache zilizopita ambapo inasemekana alifanya mazungumzo na mabosi wa Azam Fc na kukubaliana kila kitu ambapo ameshapiga mpaka picha za utambulisho klabuni hapo.

Ibenge sasa anatarajiwa kutambulishwa muda wowote klabuni hapo kwa ajili ya kujiandaa mapema na msimu mpya wa ligi kuu nchini ambapo mabosi wa Azam Fc wanataka kurejesha makali yao baada ya msimu huu kitofanya vizuri.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited