Home Makala Aucho Kupata Donge Nono

Aucho Kupata Donge Nono

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la Soka Uganda (FUFA) limeboresha maslahi ya wachezaji wake wa timu ya Taifa hasa kuelekea katika mchezo muhimu wa kufuzu Afcon ambapo awali posho ya siku ilikuwa Sh1.2 milioni ya Tanzania (Sh1.8 milioni ya Uganda) na sasa imeongezeka kufikia Sh1.8 milioni ya Tanzania.

Kutokana na mabadiliko hayo mapya pia bonasi ya mchezo wa mwisho wa kuwania kufuzu Afcon nazo zimebadilika ambapo Uganda kama itaifunga Niger na kufanikiwa kufuzu kila mchezaji na benchi la ufundi atabeba Sh12 milioni ya Tanzania.

Mechi za mwisho kundi F kufuzu Afcon 2024 zitapigwa kesho saa 4:00 usiku katika viwanja viwili tofauti ambapo Tanzania (Taifa Stars) ikiwa ugenini Algeria itasaka ushindi au sare kujihakikishia nafasi ya kufuzu huku Niger ikiikaribisha Uganda.

banner

Tanzania ina pointi saba katika kundi hilo ambapo ushindi au sare itafuzu huku Uganda ikijitaji ushindi wa mabao mengi huku ikiiombea Taifa Stars kupoteza mchezo huo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited