Home Makala Aucho Kusepa Yanga sc

Aucho Kusepa Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa klab ya Yanga, raia wa Uganda Khalid Aucho ameweka bayana Kuwa anahitaji kuondoka Klabuni hiyo iliyopo mitaa ya Twiga na Jangwani na hii ni baada ya kupokea ofa mpya kutoka moja ya klabu inayoshiriki ligi kuu nchini Saudi Arabia.

Kwa mujibu wa gazeti moja la michezo kiungo huyo Ameuomba Uongozi wa Yanga kutoongeza Mkataba unaoisha Mwishoni mwa msimu huu ambapo amevutiwa na ofa hiyo nono ya mamilioni ya fedha kutoka kwa waarabu.

Yanga sc bado hawajampa jibu staa huyo kama wanakubaliana na suala hilo ama watapandia juu ofa hiyo ili kumbakisha staa huyo kikosini kutokana na kuwa na mchango mkubwa hasa katika kujenga mashambulizi licha ya kuwa na spidi ndogo hasa katika kukaba timu inaposhambuliwa kwa kasi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited