Home Makala Beki Azam Fc Aitwa Senegal

Beki Azam Fc Aitwa Senegal

by Sports Leo
0 comments

Beki wa klabu ya Azam fc  Cheikh Tidiane Sidibe amejumuishwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Senegali ‘Simba wa Teranga’ kwaajili ya maandalizi ya mchezo mmoja wa kuwania kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2023 dhidi ya Rwanda utakaochezwa Septemba 9 mwaka huu.

Sidibe amekua mchezaji pekee anaecheza ligi kuu Tanzania Bara kujumuishwa kwenye kikosi cha Simba wa Teranga ambao  wamewaacha nyota wao wengi wa kikosi cha kwanza.

Hata hivyo tayari Senegali wamekwisha fuzu kwenda AFCON kwakuwa tayari wanaongoza kundi L wakiwa na pointi 13 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yeyote katika kundi hilo na nafasi ya pili inashikwa na Msumbiji na pointi 7, Benin pointi 5 na Rwanda pointi 2.

banner

Sidibe amesajiliwa na Azam Fc msimu huu ambapo mpaka sasa amecheza katika michezo yote ya ligi kuu na ya kimataifa akiwa na klabu hiyo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited