Home Makala Beki Nkana Kutua Yanga

Beki Nkana Kutua Yanga

by Sports Leo
0 comments

Beki wa kati wa timu ya Nkana kutoka Zambia,Musa Mohammed amekiri kufanya mazungumzo na viongozi wa Yanga kwa ajili ya kujiunga na timu hiyo kutokana na mkataba wake unaokaribia kuisha hivi karibuni.

Mkenya huyo ambaye ni nyota wa zamani wa Gor Mahia aliwahi kucheza ndani ya Kf Tirana ya nchini Albania kabla ya mwaka 2018 ambapo alijiunga na Nkana ya Zambia.

Musa amethibitisha kuwepo kwa mazungumzo baina yake na viongozi wa Yanga na iwapo mipango itaenda sawa  basi yupo tayari kujiunga nao.

banner

“Yanga kweli nimefanya nao mazungumzo kupitia wakala wangu  ambaye aliongea nao kila kitu na alinieleza walipofikia ingawa mambo hajakaa sawa kutokana na janga la Corona,ila ninayo nafasi kubwa ya kujiunga nayo kwa sababu ni timu kubwa na ninaifahamu vizuri” alisema Musa

Aliongeza kuwa mkataba wake unaisha mwezi juni na hivyo kuna uwezekano kutua Jangwani hivyo wachezaji wa Simba Sc Kama Kagere na Bocco wasitegemee urahisi ikiwa atakuwepo ndani ya Yanga Sc.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited