Home Makala Biashara United Kuhamia B.Mkapa

Biashara United Kuhamia B.Mkapa

by Sports Leo
0 comments

Biashara United haitaweza tena kucheza mechi zao za Kombe la Shirikisho Afrika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza kama ilivyokuwa mipango yao baada ya CAF kuukata uwanja huo na sasa wawakilishi hao watakipiga jijini Dar es Salaam.
Tayari timu hiyo ilishaweka kambi jijini Mwanza kwa wiki mbili, lakini juzi wameambiwa mechi yao ya awali dhidi ya FC Dikhil ya Djibouti itapigwa Benjamin Mkapa, kwa vile Kirumba imeshindwa kukidhi vigezo vilivyotakiwa.
Meneja na mratibu wa Biashara amesema wamelazimika kubadili kila kitu kwani walikuwa Kirumba kwa zaidi ya siku 10 na wachezaji walikuwa wamezoea mazingira hayo hivyo wapo kwenye hatua za mwisho za kuhamishia kambi Dar ili kuanza upya maandalizi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited