Home Makala Corona Yasababisha Juventus Wajitenge

Corona Yasababisha Juventus Wajitenge

by Sports Leo
0 comments

Wachezaji wa Juventus wote wamelazimika kujitenga kwa ridhaa baada ya kiungo wa timu hiyo,Weston McKennie kuthibitika kukutwa na Virusi vya Corona.

Weston ambaye ndiye mchezaji wa pekee wa Juventus alijiunga na klabu hiyo katika usajili wa dirisha hili akitokea  Schalke ya Ujerumani.

Kukutwa na maambukizi hayo ya Virusi vya Corona ndani ya Juventus kumewapa hofu wachezaji wote wa klabu hiyo hata kujitenga kwaajili ya kuchukua tahadhari kwani ndiye pekee aliyekutwa na virusi hivyo.

banner

Taarifa hizo zimekuja mara baada ya siku moja kupita toka Cristian Ronaldo wa Juventus athibitike pia kuambukizwa virusi hivyo akiwa kwao Ureno na sasa amejitenga chini ya uangalizi maalum wa madaktari.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited