Home Makala Hafiz Afunguka Kufunga Bao la Kwanza

Hafiz Afunguka Kufunga Bao la Kwanza

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya Yanga sc Hafiz Konkoni amefunguka kufunga bao la kwanza akiwa na timu yake mpya ya Yanga sc mara baada ya kusajiliwa na timu hiyo kuziba nafasi ya Fiston Mayele ambaye amejiunga na Pyramids Fc ya nchini Misri.

Hafiz ambaye katika mchezo huo wa kwanza wa ligi kuu kwa timu yake aliingia dakika ya 69 akichukua nafasi ya Kennedy Musonda na kufanikiwa kufunga bao la tatu akimalizia mpira uliokua unazagaa ambapo timu yake ilifunga jumla ya mabao 5-0 katika mchezo huo.

“ Kufunga bao la kwanza katika mazingira kama haya sio rahisi. Nilipokuja kwenye timu hii ya Young Africans walikuwa na mmoja wa washambuliaji bora barani Afrika, Fiston Mayele, ni presha kubwa kuziba pengo lake. Nilihitaji bao hili ili kupunguza presha, Nawaahidi kazi nzuri, ”Alisema

banner

Yanga sc ina kibarua kigumu cha kutetea makombe yake matatu msimu huu ambapo tayari wamelikosa kombe la ngao ya jamii ambalo limechukuliwa na Simba sc na sasa inawapasa kupambana kuchukua makombe ya ligi kuu na ngao ya jamii.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited