Home Makala Ihefu Yailaza Yanga sc

Ihefu Yailaza Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Ihefu Fc imefanikiwa kuchukua alama tatu kutoka kwa Yanga sc baada ya kufanikiwa kuifunga klabu hiyo kwa mabao 2-1 katika mchezo wa ligi kuu uliofanyika katika uwanja wa Highland Estates ulioko eneo la Ubaruku mjini Mbarari mkoani Mbeya.

Ikianza na mastaa wachache wanaokaa benchi akiwemo Zawadi Mauya,Salum Abubakar na Kibwana Shomari ilianza kupata bao mapema dakika ya tatu ya mchezo kupitia Pacome Zouzou akiunganisha pasi ya Clement Mzize aliyemzidi maarifa Juma Nyoso.

Bao hilo lilisawazishwa na beki Lenny Kisu dakika ya 40 baada ya makosa ya kipa Djigui Diarra ambaye alishindwa kuucheza vyema mpira uliopigwa na Never Tigere na kuupangua vibaya ambapo ulimkuta mfungaji akiwa bila kukabwa na kufunga kwa kichwa.

banner

Kipindi cha pili kilikua cha Charles Ilanfya aliyeunganisha kwa shuti kali pasi kutoka upande wa kulia mwa uwanja ambapo pamoja na juhudi za Yanga sc kutafuta goli la kusawazishwa lakini ilikua ngumu mpaka dakika tisini za mchezo zilipotamatika.

Sasa Ihefu Fc imefikisha alama sita ikisogea hadi nafasi ya saba ya msimamo wa ligi kuu nchini huku Yanga sc ikisalia katika nafasi ya pili ya msimamo ikiwa na alama tisa baada ya kucheza michezo minne ya ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited