Home Makala Kichuya Na Wengine Sita Kuikosa Fainali FA

Kichuya Na Wengine Sita Kuikosa Fainali FA

by Dennis Msotwa
0 comments

Simba Sc inatarajiwa kucheza fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Namungo fc siku ya Jumapili Agosti 2, Uwanja wa Nelson Mandela

Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa timu zote kupambania taji hilo muhimu kwani timu itakayo shinda na kunyakua kombe ndiyo itakayo iwakilisha nchi kwenye michuano ya kimataifa kwenye Kombe la Shirikisho.

Patrick Rweyemamu amabaye ni meneja wa Simba amesema kuwa kikosi ambacho kilikwenda Tanga kucheza na Coastal Union kisha kikamalizana na Polisi Tanzania kule Moshi ndicho ambacho kitaelekea Sumbawanga.

banner

Wachezaji ambao walikosa michezo hiyo miwili na inatarajiwa watakosa fainali ni Ibrahim Ajib, Sharaf Shiboub, Rashid Juma, Haruna Shamte, Shiza Kichuya, Cyprian Kipenye na Tairone Santos.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited