Home Makala Kipigo Chamkosesha Madili Mwakinyo

Kipigo Chamkosesha Madili Mwakinyo

by Dennis Msotwa
0 comments

Bondia Matanzania Hassan Mwakinyo ameelezea masikitiko yake juu ya kipigo cha Tko raundi ya nne kutoka kwa Bondia Mwingereza Liam Smith katika pambano lililofanyika Septemba 4 jijini Liverpool nchini Humo.

Akizungumza na mwandishi Millard Ayo kupitia Kipindi cha Amplifier Mwakinyo amesema kuwa pambano hilo lilikua na nafasi ya kubadilisha sehemu kubwa ya maisha yake kama angeshinda ambapo angevuna pesa ndefu lakini pia angepata pambano jingine lenye pesa ndefu zaidi ambazo zingemtoa katika umaskini.

“Nimekosa hela nyingi sana kutokushinda lile pambano, lakini sijawahi kukata tamaa na silaumu mipango ya Mungu. Ningeweza kuuaga umasikini. Ningeweza kukodisha bodaboda wote wa Tanga, kila mmoja ningempa bajaji tano halafu angekuwa ananirudishia hela kwa namna anayotaka mwenyewe.” ameeleza Hassan Mwakinyo.

banner

Mwakinyo licha ya kupoteza pambano hilo bado ameendelea kushikilia nafasinza juu katika uzani wa kati duniani ambapo barani Afrika akishika nafasi ya pili na nafasi ya sita duniani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited