Home Makala Kiungo Fundi Aikacha Simba sc,Atua Singida Big Stars

Kiungo Fundi Aikacha Simba sc,Atua Singida Big Stars

by Sports Leo
0 comments

Licha ya kufanya mazungumzo na Simba sc na kuelewena kila kitu kiungo Kelvin Nashon ametua katika klabu ya Singida Big Stars akitokea klabu ya Geita Gold Sc baada ya timu hiyo kununua mkataba wake uliokua umesalia klabuni hapo.

Nashon tayari ameshajiunga na kambi ya klabu yake hiyo mpya iliyoko visiwani Zanzibar katika michuano ya kombe la mapinduzi na alikuwapo katika kikosi cha akiba cha mchezo dhidi ya Azam Fc.

Taarifa zinadai kuwa Singida Big Stars wamekamilisha usajili wa kiungo huyo baada ya kufikia makubaliano na klabu ya Geita Gold sc huku wakitoa dau zuri kushinda lile la Simba sc huku mchezaji nae akipewa dau zuri lililomvutia kujiunga na matajiri hao.

banner

Simba sc ilishafikia makubaliano na mchezaji huyo kuhusu dau la usajili na mshahara huku ilikua imebakiwa na vitu vichache vya kimkataba ili kukamilisha dili hilo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited