Juventus imethibitisha kuachana na kocha mkuu , Maurizio Sarri baada ya kudumu kwa msimu mmoja ndani ya klabu hiyo.
Sarri ndani ya msimu wa 2019/20 alifanikiwa kutwaa taji la Serie A ila kilichopelekea kutimuliwa kwenye klabu hiyo ni kutokana na kuishia hatua ya 16 bora kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Pia kupoteza mbele ya Lyon kwenye mchezo wa usiku wa jana kuamkia leo kumewakasirisha zaidi mabosi wa Juventus kwani walifungwa mabao 2-1 na kuwapa nafasi Lyon ya kusonga mbele hatua ya nusu fainali kwa faida ya bao la ugenini.