Home Makala Lamine Wa Yanga Hadi 2023

Lamine Wa Yanga Hadi 2023

by Sports Leo
0 comments

Yanga Sc kupitia kwa mkurugenzi wa uwekezaji wa GSM,Hersi Said wamethibitisha kumuongezea mkataba beki wao wa kimataifa,Lamine Moro ambaye iliripotiwa kuwa mkataba wake unakaribia kufikia ukingoni msimu ujao 2021.

Lamine alijiunga na wanajangwani hao kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Bidcon ya Zambia na kutokana na uwezo wake ndani ya uwanja mabosi hao wameamua kumpa dili jipya hivyo atabakia Yanga hadi mwaka 2023.

Ndani ya ligi kuu bara amecheza mechi tatu msimu wa 2020/21 amefunga mabao mawili akiwa ni kinara wa kutupia mabao ndani ya Yanga iliyofunga mabao manne ikiwa imecheza mechi nne.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited