Home Makala Man Utd Yasajili Straika Hatari

Man Utd Yasajili Straika Hatari

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Manchester United imethibitisha kufikia makubaliano na klabu ya Wolves juu ya kumsajili mshambuliaji Matheus Cunha kwa ada ya uhamisho ya pauni Milioni 62.5 ili kujiweka sawa na msimu ujao baada ya kuchemsha msimu huu.

Uhamisho wa mshambuliaji huyo raia wa Brazil unatarajiwa kukamilika rasmi baada ya kukamilika kwa visa yake na usajili baada ya kurejea kutoka kwenye majukumu na timu ya taifa ya Brazil.

banner

Cunha (26) raia wa Brazil amekubali kusaini mkataba wa miaka mitano na nyongeza ya mwaka mmoja zaidi huku akitarajiwa kuvaa jezi namba 10 iliyokuwa ikivaliwa na Marcus Rashford ambaye anatarajiwa kuondoka klabuni hapo kwenye dirisha la majira ya kiangazi.

Tayari klabu hiyo imetoa taarifa rasmi ya kuhusu kumsajili  nyota huyo anayemudu kucheza kama mshambuliaji au kiungo mshambuliaji ambapo taarifa hiyo mesema “Manchester United imefikia makubaliano na Wolves juu ya uhamisho wa Matheus CCunha”,ilisomeka taarifa hiyo

Msimu klabu hiyo imetoka kama katika michuano yote iliyoshiriki huku ikimaliza ligi kuu katika nafasi ya 16 ikiwa ni poromoko kubwa zaidi klabuni hapo katika ligi kuu ya soka nchini Uingereza.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited