Home Makala Masoud Djuma Kocha Mpya Dodoma Jiji

Masoud Djuma Kocha Mpya Dodoma Jiji

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya soka ya Dodoma jiji Fc yenye makao yake makuu jijini Dodoma imemuajiri kocha wa zamani wa klabu ya Simba sc Masoud Djuma kama kocha mkuu waklabu hiyo kufuatia kuachana na kocha Mbwana Makata.

Djuma anachukua nafasi hiyo baada ya Makata kutimuliwa klabuni hapo kutokana na matokeo mabovu ambapo timu hiyo Ndani ya michezo mitano iliyopita, Makata alijikuta akiongoza Dodoma Jiji kuambulia pointi moja tu dhidi ya Geita Gold na kukumbana na vipigo vinne, ikiwemo vitatu mfululizo ambavyo ni kama vilikoleza kuota nyasi kwa kibarua chake makao makuu ya nchi.

Makata ambaye Mchezo wa mwisho kukaa kwenye benchi ilikuwa ni Februari 20 uliochezwa Uwanja wa Azam Complex na ubao ulisoma KMC 2-0 Dodoma Jiji nafasi yake inachukuliwa na kocha huyo ambaye ametambulishwa rasmi klabuni hapo akiwa na kazi ya kupandisha kiwango cha timu hiyo katika duru la pili la ligi kuu nchini.

banner

Dodoma jiji hivi sasa ipo katika nafasi ya 11 ya msimamo wa ligi kuu nchini ikiwa na alama 17 katika michezo 15 ya ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited