Home Makala Mayele Awalaza Geita Gold Fc

Mayele Awalaza Geita Gold Fc

by Sports Leo
0 comments

Muuaji Fiston Kalala Mayele ameendeleza moto wake wa kuzifumania nyavu baada ya kufunga bao katika ushindi wa bao 1-0 iliopata klabu yake ya Yanga sc dhidi ya klabu ya Geita Gold Sports mchezo uliofanyika katika uwanja wa Ccm Kirumba jijini Mwanza.

Yanga sc ikiwa inawakosa mastaa kama Khalid Aucho,Saido Ntibanzokiza,Jesus Moloko,Yacouba Sogne na Chico Ushindi ilianza mchezo kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la mapema kupitia kwa Mayele sekunde  ya 33 akiunganisha mpira wa kichwa ambao walinzi wa Geita Fc walizembea kuokoa na Mayele akafunga likiwa bao lake la 10 kwa msimu huu wa ligi kuu nchini.

Yanga sc ilikutana na upinzani mkali kutoka kwa Geita Gold Fc ambao walifunguka muda wote wa mchezo wakishambulia na kukaba kwa nguvu huku mshambuliaji wao George Mpole akikosa mabao ya wazi kutokana na kukosa utulivu.

banner

Yanga sc sasa imefikisha alama 45 ikiwa kileleni mwa msimamo wa ligi kuu huku ikiwa imecheza jumla ya michezo 17 huku Simba sc wakiwa katika nafasi ya pili ya msimamo wakiwa na alama 34.

Yanga sc sasa itawavaa Kmc siku ya 16 machi mwaka huu huku ikiwa na kumbukumbu ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika mchezo wa awali uliofanyika mkoani Songea.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited