Home Makala Mbeligiji Kumrithi Zahera

Mbeligiji Kumrithi Zahera

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc ipo mbioni kumshusha kocha Luc Aymael raia wa ubeligiji kuja kuifundisha timu hiyo akichukua nafasi ya Mkongo Mwinyi Zahera aliyetimuliwa klabuni hapo.

Kocha huyo anakuja kuchukua nafasi hiyo ambayo ilikua ikikaimiwa na Bonifasi Mkwasa kwa miezi takribani miwili ambaye alikua akisaidiwa na Said Maulid.

banner

Taarifa zinaeleza kocha huyo mpya ni kocha mwenye uzoefu wa soka la Afrika akifundisha soka katika vilabu vya AS Vita, AFC Leopard, Rayon Sports, Al Nasr, El – Merreikh, Polokwane na Black Leopard.

Licha ya kufundisha vilabu hivyo pia alitwaa makombe mbali mbali kama ifuatavyo:

1. League championship DR Congo akiwa na AS Vita Club (2010),

2. Gabon akiwa na Missile FC (2012).

3.Pia alishinda National Super cup nchini DRC akiwa na AS Vita Club(2011),

4. National cup akiwa na AFC Leopards Kenya (2013),

5. Alishinda kombe la  South African Nedbank cup na  Free State Stars (2018),

6. Alishinda Ke Yona Nebbank Super cup 2018

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited