Home Makala Mkenya Avutiwa Na Uwezo Wa Papy,Fei Toto

Mkenya Avutiwa Na Uwezo Wa Papy,Fei Toto

by Sports Leo
0 comments

Kiungo anayekipiga ndani ya Klabu ya Kariobang Sharks ya Kenya,Yidah Sven anavutiwa na uwezo wa kiungo Papy Tshishimbi na Fei Toto ambao wanakipiga Yanga jambo ambalo litampendeza akiungana nao.

Nyota huyo alipata nafasi ya kucheza na wachezaji hao kwenye mchezo wa siku ya Wanachi Uwanja wa Taifa ambapo ulikamilika kwa sare ya kufungana bao 1-1 na sasa inaelezwa kuwa mabosi wa Yanga wanaiwinda saini ya kiungo huyo ambaye anakaribia kumaliza mkataba wake ndani ya Sharks.

“Nipo tayari kutua ndani ya Klabu ya Yanga kwani ni timu kubwa ambayo kila mmoja atapenda kucheza bila mashaka yoyote pia nitakuwa na uwezo wa kuwatambua baadhi ya viungo wanaokipiga Yanga ikiwa ni pamoja na Fei na Tshishimbi hawa wapo vizuri nitafurahi iwapo nitapata nafasi ya kucheza nao,” alisema Sven

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited