Home Makala Morrison Agoma Simba sc

Morrison Agoma Simba sc

by Dennis Msotwa
0 comments

Baada ya kusimamishwa kwa tuhuma za utovu wa nidhamu ndani ya klabu ya Simba sc na kutakiwa kuandika barua ya maelezo kwa Afisa Mtendaji mkuu wa klabu ya Simba sc Babra Gonzalez bado Benard Morrison hajaandika barua hiyo.

Kwa mujibu wa meneja wa habari na mawasiliano wa klabu hiyo Ahmed Ally ni kwamba mpaka sasa bado mchezaji huyo hajaandika kutoa maelezo kama alivyoelekezwa kufanya na uongozi wa klabu hiyo.

Morrison alijiunga na klabu ya Simba sc baada ya kushinda kesi dhidi ya klabu yake ya zamani ya Yanga sc katika kamati ya Sheria na hadhi za wachezaji huku Yanga sc waliamua kukimbilia katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi wa michezo (Cas) ambapo mchezaji huyo alishinda.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited