Home Makala Morrison Atajwa Kutua Simba Sc

Morrison Atajwa Kutua Simba Sc

by Sports Leo
0 comments

Inaelezwa kuwa nyota wa Yanga, Bernard Morrison anaweza kuonekana akiwa kwenye uzi mweupe na mwekundu kwani tayari amemalizana na uongozi wa Smba hivyo mda wowote anaweza kutangazwa.

Mkurugenzi wa Uwekezaji ndani ya GSM ,Hersi Said ambao pia ni wadhamini wa Yanga amesema kuwa inashangaza kwani Morrison bado ana mkataba na kesi yake bado inasikilizwa, hivyo itakuwa ni ajabu kutangazwa kuwa ni mchezaji wa simba wakati kamati inafuatilia mambo yaliyopo.

“Ni muda mrefu viongozi wa Simba wamekuwa wakimlaghai ili kumpa mkataba hivyo kama atatangazwa kuwa ni mchezaji rasmi wa Simba Sc basi itatoa picha kwamba Simba walikuwa nyuma katika haya,” amesema Hersi Said

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited