Home Makala Musonda,Yanga sc Mambo Fresh

Musonda,Yanga sc Mambo Fresh

by Sports Leo
0 comments

Taarifa kutoka nchini Zambia zinadai kwamba Klabu ya Yanga ipo mbioni kukamilisha usajili wa mshambuliaji Kennedy Musonda kutoka klabu ya Power Dynamos ya nchini humo kwa dau dola laki moja ambazo ni zaidi ya  shilingi milioni 230 za kitanzania.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Zambia mwenye umri wa miaka 29, msimu huu amefunga jumla ya magoli 11 katika mechi 17 alizocheza na alikua na ofa kubwa ya kujiunga na klabu za Tp mazembe na Simba sc lakini taarifa zinadai kuwa Yanga sc imefanikiwa kushinda mbio hizo.

Staa anatarajiwa kuwasili nchini wiki ijayo tayari kukamilisha dili hilo ambapo anakuja kusaidiana na mshambuliaji Fiston Kalala Mayele katika eneo la mbele huku Heritier Makambo akitajwa kuwa ataondoka klabuni hapo kumpisha baada ya kushindwa kuonyesha makeke tangu asajiliwe na kumuachia ufalme Mayele.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited