Klabu ya Simba Sc imetangaza kuachana na mshambuliaji Leandre Willy Esomba Onana baada ya kufikia makubaliano baina ya pande zote mbili kuachana kwa maslahi yao wote.
Onana aliyesajiliwa na Simba sc akitokea klabu ya Rayon Sports ya Rwanda ambapo aliibuka mfungaji bora msimu wa 2022/2023 na kuwavutia mabosi wa Simba Sc walioamua kuvunja benki kumsajili.
Msimu uliopita Onana hakua na msimu mzuri klabuni humo akishindwa kuwashawishi walimu Roberto Oliveira “Robertinho” na Abdelhack Benchika na kuishia kuwekwa benchi mara kwa mara.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Msimu huu Mwalimu Fadlu Davis ameridhia kuondoka kwa Onana ambaye anakwenda kujiunga na klabu Al Ahly Benghazi ya nchini Libya.