Home Makala Pacha wa Maxi Kutua Yanga Sc

Pacha wa Maxi Kutua Yanga Sc

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga imenogewa na biashara na wachezaji kutoka DR Congo na sasa iko kwenye hatua za mwisho kumsaini winga fundi kutoka Union Maniema, Basiala Agee (25) ambaye alikua ni pacha wa Maxi Nzengeli klabuni hapo.

Kwenye Ligi ya Congo sasa Basiala amefanikiwa kufunga mabao matano na kutoa asisti tano huku akiwa amekosa mechi mbili za mwisho kutokana na maaamuzi viongozi wakijiandaa kumruhusu aondoke kuanza maisha mapya na Mabingwa wa nchi, Yanga SC.

Inasemekana kuwa usajili wa staa huyo unakuja kuchukua nafasi ya Jesus Moloko ambaye kocha Miguel Gamond hajaridhika na ufanisi wake hivyo anaona ni bora apishe usajili mpya katika nafasi hiyo.

banner

Mpaka sasa Yanga sc imemtambulisha Shekhan Hamis kiungo iliyemsajili kutoka Jku ya Zanzibar ikiwa ni usajili wake wa kwanza katika dirisha dogo la usajili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited