Home Makala Pamba Jiji Fc Yaoga Mamilioni

Pamba Jiji Fc Yaoga Mamilioni

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Pamba Jiji Fc imekabidhiwa fedha taslimu shilingi milioni 10 kutoka kwa uongozi wa klabu hiyo ikiwa ni hamasa kuelekea mchezo wa kesho ijumaa dhidi ya Yanga sc.

Zawadi hizo zimekabidhiwa na Naibu Meya wa Jiji la Mwanza na Mwenyekiti wa klabu hiyo Mh.Bhiku Kotecha ambapo mastaa wa klabu hiyo walikua mazoezini kujiandaa na mchezo huo katika uwanja wa Ccm Kirumba jijini Mwanza.

banner

“Tunawashukuru mashabiki kwa kuwa pamoja na sisi katika nyakati zote tulizopitia na tunawaahidi kesho watafurahi kwa kuwa tumejiandaa vizuri”Alisema mchezaji Pauline Kasindi wakatia akizungumzia kuhusu maandalizi ya timu hiyo kwa ujumla kuelekea mchezo huo.

Naye Kocha wa klabu hiyo Fred Felix Minziro alisema kuwa “Tunakutana na timu bora na sisi tutakuja na mbinu mbadala kuhakikisha tunapata ushindi kwenye mchezo huu muhimu”,Alimalizia kusema Minziro.

Pamba jiji itakua na wakati mgumu ikiwavaa Yanga sc ambao wametoka kuifunga Mashujaa Fc mabao 5-0 ugenini mkoani Kigoma.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited