Home Makala Pogba Kuzua Balaa Ulaya

Pogba Kuzua Balaa Ulaya

by Sports Leo
0 comments

Inter Milan imeingia kwenye bato la timu nne zinazopambana kumng’oa Paulo Pogba huko Manchester United kwenye usajili wa msimu ujao.

Nyota huyo Mfaransa anaonekana kuwa mguu ndani nje Man United hasa baada ya mwenyewe kukiri kutaka kwenda kutafuta changamoto mpya kwingineko.

Kocha wa Real Madrid,Zinedine Zidane kwa muda mrefu amekuwa akimtaka kiungo huyo anayeshikilia rekodi ya kusajiliwa kwa pesa nyingi ligi kuu England  lakini kuna mpango pia wa kiungo huyo kurudi Juventus mahali ambapo alishatamba  kwa miaka 4 kuanzia 2012/2016.

banner

Paris Saint-Germain pia wanataka kuinasa saini ya nyota huyo ili kucheza ndani ya Ufaransa ikiwa ni baada ya kuwauza  Neymar ndani ya Barcelona.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited