Kocha Mkuu wa Burundi ‘Intamba Mu Rugamba’, Etienne Ndayiragije amemwaacha nje ya kikosi kiungo wa Simba SC, Saido Ntibazonkiza wakati Burundi ikijiandaa kukabiliana na Namibia kwenye michezo ya kufuzu Afcon 2023 nchini Ivory Coast mwezi ujao.
Saido anatuhumiwa kwa utovu wa nidhamu baada ya kukataa kushiriki mchezo wa kirafiki dhidi ya Indonesia mapema mwezi Machi mwaka huu.
Mlinda mlango wa Coastal Union Justin Ndikumana ameitwa kikosini humo akiwa ni mchezaji pekee kutoka nchini kwa mastaa wanaocheza ligi kuu ya Nbc.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Saido amekua na matatizo ya mara kwa mara ya kinidhamu ambapo hata alipokua na Yanga sc alitemwa katika kikosi hicho baada ya kukutwa na utovu wa nidhamu kuelekea mchezo wa nusu fainali ya kombe la shirikisho dhidi ya Simba sc.