Home Makala Saido,Ambudo Watimuliwa Yanga sc

Saido,Ambudo Watimuliwa Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Taarifa kutoka mkoani Shinyanga zinasema kuwa klabu ya Yanga sc imewatimua kambini mastaa wake Saido Ntibanzokiza na Dickson Ambundo kwa kosa la kuondoka kambini bila kufuata utaratibu uliowekwa na klabu wakati timu ikiwa kambini mkoani Mwanza kabla ya mchezo dhidi ya Biashara united.

Taarifa za kutimuliwa kambini ikiwa ni siku mbili kabla kuwavaa mahasimu wao Simba sc katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la shirikisho nchini utakaofanyika katika uwanja wa Ccm Kirumba jijini Mwanza.

Uamuzi huo wa kuwatimua mastaa hao umefikiwa na kocha mkuu wa klabu hiyo Nasredine Mohamed Nabi ili kuweka nidhamu sawa kwa mastaa wote wa timu hiyo linapokuja suala la kufuata taratibu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited