Home Makala Samatta Aanza Na Sare Fenerbahce

Samatta Aanza Na Sare Fenerbahce

by Sports Leo
0 comments

Derby ya Uturuki imewakutanisha jana Galatasary na Fenerbahce ambayo anaichezea nahodha wa timu ya taifa Tanzania (Taifa Stars),Mbwana Samatta na mchuano kumalizika kwa sare ya kutofungana.

Samatta aliyejiunga Fenerbahce kwa mkopo wa mwaka mmoja akitokea Aston Villa inayoshiriki ligi kuu England aliingia dakika ya 66 kuchukua nafasi ya Mame Thiam akiwa na jezi namba 10 mgongoni.

Licha ya kuupata mpira mara chache ameonekana akisumbua timu pinzani pale ambapo anaupata mpira na amefanikiwa kuokoa mpira wa adhabu kwa kichwa uliokuwa ukitaka kutua kwenye lango lao.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited