Home Makala Simba Sc Yapotezea Mkutano na Wanahabari

Simba Sc Yapotezea Mkutano na Wanahabari

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc  haijatuma wawakilishi kwenye mkutano wa waandishi wa Habari kuelekea mchezo wake dhidi  ya Yanga sc kuzungumzia maandalizi yake ya mchezo huo unaotarajiwa kupigwa kesho Juni 25, 2025 saa 11:00 jioni kwenye Dimba la Benjamin Mkapa.

Kwa mujibu wa kanuni ni kuwa siku moja kabla ya mchezo wa ligi kuu ya Nb nchini timu zitakazo kutana kiwanjani kutuma kocha pamoja na nahodha kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari kuelezea juu ya maandalizi ya mchezo husika.

Leo Simba sc haikutuma mwakilishi yeyote licha ya juhudi za maafisa wa bodi ya ligi kuwatafuta kwa ajili ya tukio hilo.

banner

Taratibu za Ligi hiyo ni kuwa siku moja kabla ya mchezo, timu husika zinatakiwa kutuma Kocha na Mchezaji kuzungumza na Wanahabari kuhusu mchezo unaofuata ambapo ni ratiba pia inayofuatwa na Azam TV ambao wanahusika kurusha matangazo ya Ligi.

Kutokana na kukiuka kanuni hiyo sasa klabu hiyo itapigwa faini kama kanuni inavyosema.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited