Klabu ya Simba sc imekamilisha usajili wa mshambuliaji raia wa Uganda Stephen Mukwala kwa mkataba wa miaka miwili akiwa huru baada ya kumaliza Mkataba na klabu yake ya mwanzo ya Asante Katoko ya nchini Ghana.
Mshambuliaji huyo yupo kwenye kiwango bora sana hasa msimu uliopita ambapo amepata nafasi katika kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda katika kuwania kufuzu michuano ya kombe la Dunia ambapo amefunga jumla ya mabao mawili mpaka sasa.
Simba sc imelazimika kufanya kazi ya ziada kumshawishi staa huyo kutua klabuni humo kutokana na kuwa na ofa za ulama ambazo inasemekana kuwa alizikataa.
Mshambuliaji huyo anafuata nyayo za mastaa wengine wa Ugands waliowahi kusajiliwa na klabu hiyo wakiwemo Emmanuel Okwi,Juuko Murshid,George Owino na wengineo ambao baadhi leo wameacha alama klabuni hapo hasa Okwi.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Mukwala Ana kazi rahisi sana kuwania namba mbele ya Pa omar Jobe na Fredy Michael ambao bado hawajawashawishi mabosi wa timu hiyo mpaka sasa.