Home Makala Simba Sc Yasaka Kipa Mpya

Simba Sc Yasaka Kipa Mpya

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba SC inafikiria kumrudisha tena golikipa Ayoub Lakred kurudi kuitumikia klabu hiyo kuelekea msimu ujao baada ya kutoridhishwa na kiwango cha kusuasua cha kipa Moussa Camara.

Mpaka sasa suala hilo viongozi wa klabu hiyo wanasubiri ripoti rasmi ya benchi lao la ufundi ikiwa litamuhitaji Ayoub Lakred watamrudisha kikosini kuchukua nafasi ya Camara ambaye pia ameonyesha nia ya kuondoka klabuni hapo.

Pia Simba SC inamfatilia kwa ukaribu sana golikipa wa Al Hilal ya Sudan, Issa Fofana ambaye amekuwa na msimu bora sana endapo itashindwa kupatana na Lakred inaweza kumsajili kipa huyo asaidiane na Salim langoni hapo.

banner

Simba sc ilimtoa Lakred kwenye usajili wake msimu uliopita baada ya kipa huyo kuumia haloi iliyomlazimu kukaa nje ya uwanja akijitibia muda mrefu

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited