Home Makala Simba Sc,Pamba Jiji Fc Watozwa Faini

Simba Sc,Pamba Jiji Fc Watozwa Faini

by Sports Leo
0 comments

Bodi ya ligi kuu nchini imewatoza faini ya Shilingi milioni tano kila mmoja klabu za Simba sc na Pamba Jiji Fc kutokana na kuvunja kanuni siku moja kabla ya mchezo wa ligi kuu uliozikutanisha timu hizo Novemba 22 mwaka huu.

Katika mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa Ccm Kirumba jijini Mwanza na Simba sc kuibuka na ushindi wa 1-0 likifungwa kwa penati na Lionel Ateba,siku moja kabla ya mchezo kulitokea sintofahamu wakati Simba sc wakiwa mazoezini ambapo maofisa wa klabu ya Pamba Jiji walivamia mazoezi hayo na kujifungia katika moja ya vyumba vilivyopo ndani ya uwanja huo.

Maofisa wa klabu ya Simba Sc walivunja moja ya vioo vya dirisha la vyumba hivyo wakijaribu kuwatoa maofisa wa Pamba Jiji hali iliyoleta Tafrani na kusababisha Polisi kuingia kudhibiti vurugu hizo.

banner

Katika adhabu hiyo iliyotolewa na Bodi ya ligi kuu pia Simba sc inapaswa kuwasiliana na wamiliki wa uwanja kwa ajili ya kufanya ukarabati wa uharibifu huo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited