Home Makala Simba Yasajili Beki Katili

Simba Yasajili Beki Katili

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imekamilisha usajili wa beki Kennedy Juma Wilson aliyekua akichezea Singida United kwa mkataba wa miaka miwili ambapo ataitumika klabu hiyo mpaka mwaka 2021.

Beki huyo mrefu na mwenye nguvu amesajiliwa kuja kuchukua nafasi ya Salim Mbonde aliyetemwa na klabu hiyo baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu hivyo pande zote mbili kukubaliana kusitisha mkataba ama nafasi ya Juuko Murshid ambaye taarifa zinadai ataachana na klabu hiyo.

banner

Kenedy amesajiliwa kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba na Singida United aliyoichezea kwa kipindi kirefu tangu iingie ligi kuu ya Tanzania bara.

Beki huyo katili aliitwa na kocha Emmanuel Amunike lakini alitemwa katika idadi ya wachezaji waliosafiri na timu hiyo kuelekea nchini Misri katika michuano ya Afcon.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited