Kocha mkuu wa Simba SC,Sven Vandenbroeck amesema kwa sasa anakiandaa kikosi chake maalum kwa mchezo ujao wa ligi kuu bara utakaofanyika uwanja wa Mkapa dhidi ya Biashara United siku ya Jumapili.
Sven ameyasema hayo baada ya kutoa sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar katika mchezo wa jana uliofanyika katika uwanja wa Jamuhuri mkoani Morogoro.
Mchezo wa jumapili utakuwa mchezo wa kwanza kwa mabingwa hao watetezi wa ligi kuu bara kucheza katika uwanja wa nyumbani baada ya mbili zilizoisha kucheza ugenini.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Wachezaji na benchi la ufundi wamepokea changamoto katika mchezo uliyopita na wamezipokea ili kujipanga kwa mchezo ujao na kuweka mbinu mpya watakazozitumia dhidi ya Biashara United.