Home Makala Sven Akiandaa Kikosi Kwa Biashara

Sven Akiandaa Kikosi Kwa Biashara

by Sports Leo
0 comments

Kocha mkuu wa Simba SC,Sven Vandenbroeck amesema kwa sasa anakiandaa kikosi chake maalum kwa mchezo ujao wa ligi kuu bara utakaofanyika uwanja wa Mkapa dhidi ya Biashara United siku ya Jumapili.

Sven ameyasema hayo baada ya kutoa sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar katika mchezo wa jana uliofanyika katika uwanja wa Jamuhuri mkoani Morogoro.

Mchezo wa jumapili utakuwa mchezo wa kwanza kwa mabingwa hao watetezi wa ligi kuu bara kucheza katika uwanja wa nyumbani baada ya mbili zilizoisha kucheza ugenini.

banner

Wachezaji na benchi la ufundi wamepokea changamoto katika mchezo uliyopita na wamezipokea ili kujipanga kwa mchezo ujao na kuweka mbinu mpya watakazozitumia dhidi ya Biashara United.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited