Home Makala Sven Aondoka Simba sc

Sven Aondoka Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Kocha mkuu wa klabu ya Simba sc Sven Vandebroek amejiuzuru kufundisha klabu hiyo na kuondoka nchini mara moja akielekea nyumbani kwake nchini Ubeligiji.

Taarifa za awali zilidai kwamba kocha huyo alivunja mkataba wake akidai kuwa na matatizo ya kifamilia lakini taarifa rasmi kutoka klabuni hapo zinasema kuwa makubaliano ya pande zote yalifikiwa katika kuvunja mkataba na kocha huyo.

Taarifa hiyo imeonekana kuwastua wadau wa soka nchini hasa ikizingatiwa kuwa imekuja siku moja tu baada ya timu hiyo kufuzu hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited