Taarifa kutoka kwa idala ya tiba ya klabu ya Yanga, inabainisha Nahodha Papy Tshishimbi huenda akakosa mechi za mwanzo ligi itakaporejea akiuguza jeraha la goti alilopata kwenye mazoezi ya timu hiyo
Mcongomani huyo leo atawashuhudia wenzake wakijipima dhidi KMC, mchezo wa kirafiki ambao utapigwa uwanja wa Uhuru
Daktari wa Yanga Dk Shecky Mngazija, amesema Tshishimbi alipata jeraha baada ya kuteguka mguu wake wa kulia
Amesema kiungo huyo bado yupo chini ya uangalizi wa daktari hadi pale hali ya jareha lake litakapopona.
“Kwa sasa Tshishimbi yupo chini ya uangalizi wa daktari kila siku anatakiwa kuhudhuria hospitalini kuangaliwa maendeleo yake,” alisema Mngazija
Cc:Youngsportsupdates