Home Makala Waarabu Waifuata Yanga sc Dar

Waarabu Waifuata Yanga sc Dar

by Sports Leo
0 comments

Timu ya soka ya Al Hilal Tayari imeanza safari ya kuja nchini kuja kuvaana na Yanga sc mchezo wa kwanza katika hatua ya pili ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika mchezo utakaofanyika siku ya Jumamosi katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.

Katika mchezo huo ambao Yanga sc atakua mwenyeji unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kutokana na kiu ya Yanga sc kufuzu hatua ya makundi ya klabu bingwa barani Afrika huku mara ya mwisho kufuzu ikiwa ni mwaka 1998 ambapo baada ya hapo wamekua wakiangukia katika kombe la shirikisho pekee ambapo wamefika makundi mara mbili kwa miaka ya hivi karibuni.

Al Hilal imeanza safari ya kuja jijini Dar es salaam ikitokea Congo ambako iliweka kambi ya muda mfupi ya maandalizi na kufanikiwa kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Tp Mazembe na sasa hivi leo wapo njiani kuja nchini ambapo wanatarijiwa kutua jioni hii ya leo tayari kwa mechi hiyo ya keshi kutwa Jumamosi.

banner

Baada ya mchezo huo itakua ni kazi kwa Yanga sc kusafiri mpaka jijini Khartoum Sudan kuvaaana na waarabu hao ambao wanasifika kuwa na mashabiki wakorofi hasa kwa kushangilia na staili ya kuwasha moto na kupiga ngoma mwanzo mpaka mwisho wa mchezo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited